Jiwe la msingi lawekwa RRH tayari kwa kuanza ujenzi wa jengo la akina mama.


Hafla ya Uzinduzi wa jengo la Idara ya dharula Tosamaganga hospitali lililo zinduliwa na Muhashamu Baba Askofu Tarcisius J.M. Ngalalekumtwa wa jimbo la Iringa iliyofanyika mnano tarehe 12/5/2023.
Maboresho hayo makubwa yanafanywa kwa kutumia mapato ya ndani lakini pia jengo la I.C.U linajengwa kwa Michango iliyopatikana kwa Mbio za hisani za kuchangia I.C.U zilizofanyika tarehe 22 mwezi Jun mwaka 2023. hata hivyo bado kuna uhitaji wa wadau wa Afya na mashirika mbalimbali kuombwa kuchangia ujenzi wa I.C.U kwani bado hatujafikia Malengo.
Pichani ni Mtaalamu wa CT- SCAN Sr. Astrida akitoa maelezo mbele ya kamati ya siasa ya Mkoa wa Iringa Ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa kwanza upande wa kushoto Ndugu Daud Yassin akiwa ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh. Halima Dendego wa pili kutoka upande wa kushoto na viongozi wengine walipotembelea Hospitali…
Tosamaganga Regional Referral Hospital inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi kupitia ujenzi wa Jengo jipya la Mama na Mtoto, mradi mkubwa na wa kimkakati unaolenga kuinua ustawi wa afya ya wanawake na watoto katika mkoa wa Iringa na maeneo jirani. Picha inayoonekana inaonyesha hatua muhimu za ujenzi zinazoendelea kwa kasi,…